Chuo kinatoa mafunzo kwa wale wanaotaka kufanya mitihani ya taifa ya Ufundi na kupata cheti cha ufundi yaani National Vocational Awards katika hatua (level) za NVA I, NVA II na NVA III.
1. ORODHA YA KOZI (FANI) ZINAZOTOLEWA
Waombaji wanayo nafasi ya kujiendeleza katika mojawapo ya kozi (fani) zifuatazo:
A. Kampasi (Campus) ya Arusha Mjini (Main Campus)
- Biashara (Business Operation Assistant)
- Utalii (Tour Guiding)
- Ukataji na Uchongaji wa Madini (Gemstone Cutting and Polishing)
- Uchoraji wa Ramani (Civil Draughting)
- Maabara Msaidizi (Laboratory Assistant)
- Tehama (Information and Communication Technology)
- Ufundi Magari (Motor Vehicle Mechanics)
- Ufundi wa Umeme wa Magari (Auto Electrical)
- Ufundi wa Umeme wa Majumbani (Domestic Electrical Installation)
- Ufundi Electroniki (Electronics)
- Ufundi Ujenzi (Masonry and Brick Laying)
- Ujenzi na ukarabati wa barabara (Road Construction and Maintenance)
- Ufundi Selemara (Carpentry and Joinery)
- Ufundi wa Viyoyozi na Majokofu (Refrigeration and Air Conditioning)
- Ufundi Mitambo (Fitter Mechanics)
- Ufundi wa Uchomeleaji na Uhunzi wa Vyuma (Welding and Metal Fabrication)
- Ufundi Bomba (Plumbing and Pipe Fitting)
- Ufundi wa Uchongaji wa Vyuma na Vipuli (Fitting and Machining)
B. Kampasi (Campus) ya Kikuletwa
- Ufundi Bomba (Plumbing and Pipe Fitting)
- Ufundi Ujenzi (Masonry and Brick Laying)
- Ufundi wa Umeme wa Majumbani (Domestic Electrical Installation)
- Ufundi wa Mitambo ya Uzalishaji wa Umeme wa Maji (Hydropower Plants Maintenance)
- Ufundi wa Umeme wa Mfumo wa Jua (Solar Energy)
- Ufundi wa Umeme wa Mfumo wa Nishati Taka (Bio-Energy)
- Ufundi wa Umeme wa Mfumo wa Upepo (Wind Energy)